Sunday, 27 October 2013

UPDATES: INASIKITISHA SERENGETI FIESTA YAISHA KWA AIBU KUBWA, WASANII KIBAO HAWAJAPANDA KWA STAGE AKIWEMO MOHOMBI,DIAMOND,CHEGE N.K...!


Usiku wa kuamkia leo pale leaders Club jijini Dar es Salaam Palikuwa hapatoshi kulikuwa na nyomi ya kufa mtu wakipata Raha za Fiesta ila Gafla Majira ya saa 10 usiku Umeme Ukazima gafla Wakati Ommy Dimpoz akiwa jukuani na J.Martins kutoka Nigeria na kusababisha show hiyo iishie hapo.
Wengi Wamelalamika kwa Sababu Wasanii Wengi akiwemo Diamond,Chege,Temba,Madee,Afande Sele na Wengine Kibao hawajafanya show Wakati walikuepo kwa Ratiba.Kama Vile

haitoshi hata Msanii kutoka Sweden Mahombi hajafanikiwa kufanya show.Watu wamesubiri mpaka saa 11 alfajiri hatimaye wakakata tamaa na kuanza kuondoka huku lawama nyingi zikienda kwa Waandaaji kwa kutojipanga Vizuri.
Watu kiukweli walijaa sana na wamepata adhabu ya kusimama zaidi ya Masaa 10 kwa sababu kulikuwa hakuna Viti wala mahali pa kukaa hivyo ukiingia ndani ni kusimama mpaka show inaisha.
Kitu kingine kibaya ni kujaa kwa Wauni wengi nje ya ukumbi nawatu wameporwa vitu vyao hadharani tena kwa nguvu.
Maoni yangu kwa Waandaaji ni kujipanga ili kuepushana na Aibu waloipata Mwaka huu!!

No comments:

Post a Comment